Find Your Dream Job Today

NAFASI ZA KAZI YA UALIMU | GOD’S BRIDGE SECONDARY

Posted:  |  Deadline: Checking... Loading

GOD’S BRIDGE DEVELOPMENT FOUNDATION (GBDF)
GOD’S BRIDGE SECONDARY SCHOOL (GBSS)
P.O. BOX 22, TUKUYU – MBEYA
Simu: +255 (0)743 122428


TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA UALIMU

UTANGULIZI

Shule ya Sekondari GOD’S BRIDGE ni kati ya shule zinazomilikiwa na kuendeshwa na God’s Bridge Development Foundation Co. Ltd. Shule inaendeshwa kwa misingi ya imani ya Kanisa la Waadventista Wasabato, ikiwa na wanafunzi kuanzia Kidato cha I hadi cha VI.
Shule ipo Km 6 kutoka Barabara Kuu ya Mbeya–Malawi, karibu na KKK Jirani na Chuo cha Magereza Kiwira.


NAFASI ZA KAZI

Uongozi wa Shule ya Sekondari GOD’S BRIDGE unawatangazia nafasi za kazi ya ualimu katika masomo yafuatayo:

  1. PHYSICS (FIZIKIA) – Nafasi 01 (O-Level & A-Level)

  2. ENGLISH (KIINGEREZA) – Nafasi 01 (O-Level & A-Level)

  3. GEOGRAPHY (JIOGRAFIA) – Nafasi 01 (O-Level & A-Level)

  4. KISWAHILI – Nafasi 01 (O-Level & A-Level)


SIFA ZA MUOMBAJI NA MAANDALIZI ANAYOTAKIWA KUYAFANYA

Mwombaji anatakiwa kuwa na:

  • Elimu ya ngazi ya Shahada ya Ualimu katika somo husika

  • Barua ya Maombi

  • Vyeti halisi pamoja na vivuli vyake

  • Wasifu Binafsi (CV)

  • Uwezo wa kuandika (kutakuwa na mtihani)

  • Mpango wa somo la kufundishia (Lesson Plan)


USAILI

Usaili utafanyika katika Shule ya Sekondari GOD’S BRIDGE – Tukuyu.
Muda wa usaili utaanza saa 2:00 asubuhi kulingana na ratiba ifuatayo:

RATIBA YA USAILI

Siku/TareheSomo
Jumanne, 13/01/2026Physics (Fizikia)
English (Kiingereza)
Geography (Jiografia)
Kiswahili

Imetolewa na:
MUSA LUSATO
MKUU WA SHULE

Tarehe: 28/12/2025




How to Apply

Please read the instructions above on how to apply.

Join our community for more updates, and tips: